Thursday, October 30, 2008

siku inakuja Afrika itaungana,siku inakuja waafrika wote waishio ughaibuni watarudi nyumbani

maneno yake Nabii Marcus Garvey
ndoto ambayo bado haijatimia lakini muda si mrefu maneno yake nabii Marcus Garvey yatatimia,itakuwa siku ya furaha sana pale tutakuwa ufukweni kuwapokea ndugu zetu kutoka ughaibuni,itakuwa siku ya furaha kwani tutawakaribisha nchi ya ahadi SHASHAMANE.
naamini katika nguvu na uwezo wa aliye hai Mfalme haile sellasi i atafanikisha Afrika iungane na kuwa kitu kimoja,naamini siku inakuja Afrika itakuwa na amani na upendo,naamini siku inakuja Afrika haitakuwa na maskini wala tajiri.bado naamini mimi na mimi unapenda sana.
Hivi naomba kuuliza,eti ni vigumu kusoma shahada ya udhamili hapa Afrika?au nauliza tena eti nivigumu kusoma katika mazingira ya hapa nyumbani mpaka uende kusoma nje?sasa nami nashangaa pake mzaliwa wa afrika anapokuja kutalii nchi yake.Eti ukijuwa lugha za kigeni kuliko lugha za nyumbani ni sifa ehhhh.

No comments: